TAARIFA KWA UMMA
Kufuatia juhudi kubwa zilizofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ofisi ya Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGOs) na Baraza la Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NaCoNGO) katika kutatua mgogoro uliokuwepo UMATI, napenda kuutarifu umma kuwa wanachama hai na wenye mapenzi mema na Shirika la Chama cha Uzazi na Malezi Bora Tanzania (UMATI) walifanikiwa kupitia na kuidhinisha Katiba na Kanuni za Shirika zinazozingatia Sheria na miongozo ya uendeshaji wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali.
Mchakato huu uliwezesha kufanyika mikutano kadhaa ukiwemo wa uchaguzi wa viongozi wa wanachama kwa kuzingatia katiba na kanuni za shirika la UMATI pamoja na sheria na miongozo ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali. Kwasasa Shirika la UMATI lina uongozi halali kwa mujibu wa katiba ambao ni Mwenyekiti, Katibu, na Mweka Hazina.
Aidha, ninapenda kutoa taarifa kuwa uongozi uliopo uliitisha Mkutano Mkuu tarehe 9 Januari 2026, ambapo pamoja mambo mengine, ulichagua wajumbe 7 wa Bodi ya Wagurugenzi wa Shirika kwa kuzingatia Sheria na Miongozo ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali na kwa kuzingatia viwango vya utawala bora vya International Planned Parenthood Federation (IPPF). Wajumbe hao walichaguliwa kwa kuzingatia uzoefu wao wa kitaaluma na utaalamu katika maeneo ya sheria, ukaguzi wa hesabu ya fedha, mawasiliano, afya, utawala bora, na uhamasishaji wa rasilimali.
Bodi ya Wakurugenzi imefanikiwa kupatiwa mafunzo ya awali (induction) ambayo yalifanyika tarehe 20 na 21 Januari 2026 kwa kushirikiana na wakufunzi kutoka IPPF.
Aidha, Uongozi wa UMATI unapenda kuutaarifu umma kwamba kumekuwepo na taarifa za upotoshwaji na tuhuma mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii zilizolenga kulichafua Shirika letu, Ofisi ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali pamoja na NaCoNGO kuwa Shirika linajihusisha na miradi isiyofuata maadali na tamaduni za nchi. Kwa taarifa hii, napenda kutoa taarifa kuwa, habari hizo hazina ukweli wowote na kwamba shirika limetoa taarifa kwa vyombo husika na zinafanyiwa kazi ili hatua stahiki za kisheria zichukuliwe.
Mwisho, napenda kuwataarifu kuwa, kwasasa UMATI ina jumla ya wanachama hai wapatao 51 ambayo orodha yao imeambatinishwa na taarifa hii. Napenda kumshukuru Muheshimiwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali pamoja na Uongozi wa NaCoNGO kwa juhudi kubwa walioifanya kuhakikisha UMATI inasimama imara na kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa kuchangia juhudi za serikali na kuwafikisha hutuma Watanzania.
Pia, natoa shukrani za dhati kwa wanachama hai wa UMATI kwa juhudi zao katika kuhakikisha Shirika hili linaendele kuimarika na kuendelea majukumu yake.
Wenu katika Ujenzi wa Taifa.
Majina ya Wanachama Hai
| S/N | Name |
| 1 | David M Lucas |
| 2 | Abdallah Jafari Chaurembo |
| 3 | John Maliyapamba Komba |
| 4 | Agatha Peter Haule |
| 5 | Benedicta Josephine Sinzo Maganga |
| 6 | Thabit Badi Lema |
| 7 | Husna Boniface Wangwe |
| 8 | Esteria Joachim Kisoka |
| 9 | Latifu Abdulrahmani Saidi |
| 10 | Sosthenes Stephen Amasi |
| 11 | Laurencia Enock Ndali |
| 12 | Kassimu Omari Abdallah |
| 13 | Alice Robert Mwantobe |
| 14 | Magdalena Honest Kawishe |
| 15 | Gertrude Nicodem Naphtali |
| 16 | Angel Lucas Pinda |
| 17 | Grace Christopher Masawe |
| 18 | Jamali Juma Kimbo |
| 19 | Pius John Isaack |
| 20 | Rehema Athuman Nkungu |
| 21 | Gerald Vitus Kihwele |
| 22 | Kabora Elisha Kabora |
| 23 | Fredinandy Sylvester Nyamonge |
| 24 | Issaya Jacobo Laizer |
| 25 | Yahaya Kwatta Hussein |
| 26 | Herry Eliufoo Christopher |
| 27 | Fidelis John Owenya |
| 28 | Priscus Tarimo |
| 29 | Maiko Joseph Ernest |
| 30 | Mpeligwa Gwakisa Emmanuel |
| 31 | Hafidhi Yahaya Lumbi |
| 32 | David Joseph Mwamwaja |
| 33 | Linda Raphael Kyando |
| 34 | Prince Gwamaka Mwaihojo |
| 35 | Edmund E. Mwandebwa |
| 36 | Richard A. Kajala |
| 37 | Saidi Mussa Nyengedi |
| 38 | Charles Mashilanga Mashilanga |
| 39 | Charles NtwaleLlukas |
| 40 | Mufandii Hamisi Msaghaa |
| 41 | Norbert Faustus Masebe |
| 42 | Bernard Emmanuel Yombayomba |
| 43 | Anastazia Kifuku |
| 44 | Bibiana Afred Kasochela |
| 45 | Charles Simon Yakusola |
| 46 | Moses Bonifas Kandege |
| 47 | Daniel David Mtamakaya |
| 48 | Zenna Hussen haji |
| 49 | Cuthbert David Maendaenda |
| 50 | Mohamed Mustapha |
| 51 | Julius Samweli Madiga |
Kwa maelezo zaidi Pakua Barua rasmi ya Taarifa hii: Hapa





